Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021Mfano

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

SIKU 4 YA 31

Yesu anaonyesha kwamba ndiye Masihi aliyetumwa na Mungu, ijapokuwa Wayahudi waliomsikia hawakutambua hilo. Shamba la mizabibu ni taifa la Israeli. Imeandikwa kwa mfano katika Isa 5:7, Shamba la mizabibu la Bwana wa majeshi ndilo nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni mche wake wa kupendeza; akatumaini kuona hukumu ya haki, na kumbe! Aliona dhuluma; alitumaini kuona haki, na kumbe! Alisikia kilio. Mwenye shamba ni Mungu. Wakulima ni mfano wa hao Wayahudi alioongea nao Yesu, na watumwa ni manabii waliotumwa na Mungu. M.9 una maonyo kwa Wayahudi waliosukumia mbali neema ya Mungu: Yule bwana wa shamba la mizabibu … atakuja na kuwaangamiza wale wakulima, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine. M.10 waonyesha kwamba Yesu ni msingi. “Jiwe kuu la pembeni” ni mfano kuhusu Yesu. Lakini pamoja na hilo, bado watu wengi na hata wakubwa wa jamii wanamkataa. Wewe je, imani yako iko katika msingi gani?

siku 3siku 5

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu k...

More

Tungependa kuishukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha