Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku 12Mfano

Soma Biblia Kila Siku 12

SIKU 30 YA 31

Waisraeli wanapokutana ili kuabudu, wana sababu ya kumsifu Mungu. Licha ya kuwa Mwumbaji wao, yeye pia ni mfalme wao awapambaye kwa wokovu.Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake, huwapamba wenye upole kwa wokovu(m.4). Wao ni wajumbe wa Mungu wanaoeneza utawala wake kwa wanadamu wote. Lakini kama utawala wa Mungu unataka kuenezwa duniani, ni lazima waasi waadhibiwe kwanza. Kwa hiyo hukumu juu ya maadui zake ni sababu ya sifa ya Mungu. Wajibu wa Mkristo wa leo ni kuwa mjumbe wa habari njema za Yesu, Bwana na Mwokozi wetu, kwa watu wote ili waache maasi.

siku 29siku 31

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 12

Soma Biblia Kila Siku 12 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kitabu cha Mwanzo, Mathayo, 2 Wa...

More

Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha