1
Waroma 6:23
Swahili Roehl Bible 1937
SRB37
Kwani mshahara wa ukosaji ni kufa; lakini gawio, Mungu analotupa katika Bwana wetu Kristo Yesu, ni uzuma wa kale na kale.
Linganisha
Chunguza Waroma 6:23
2
Waroma 6:14
Kwani ukosaji hautashika ufalme, uwatawale, maana nguvu yenu siyo ya Maonyo, ila ya upole.
Chunguza Waroma 6:14
3
Waroma 6:4
Hivyo tulizikwa pamoja naye tulipobatiziwa, tufe naye, ni kwamba: Kama Kristo alivyofufuliwa katika wafu kwa nguvu ya utukufu wa Baba, vivyo nasi sharti tupate upya wa maisha, tuendelee nao.
Chunguza Waroma 6:4
4
Waroma 6:13
Wala msivitoe viungo vyenu, viwe mata ya upotovu ya kuyatumikia makosa! Ila mjitoe wenyewe kumtumikia Mungu kwa hivyo, mnavyoishi, tena mlikuwa mmekwisha kufa! Navyo viungo vyenu mvitoe, viwe mata ya wongofu ya kumtumikia Mungu!
Chunguza Waroma 6:13
5
Waroma 6:6
Kwani tunalitambua neno hili: mtu wetu wa kale amewambwa msalabani pamoja naye, miili yetu yeye kukosa ipate kukomeshwa, sisi tusiyatumikie tena makosa kama watumwa.
Chunguza Waroma 6:6
6
Waroma 6:11
Nanyi jiwazieni hivyo: makosa mmekwisha kuyafia, lakini sasa mnaishi, mmtumikie Mungu katika Kristo Yesu!*
Chunguza Waroma 6:11
7
Waroma 6:1-2
Sasa tusemeje? Tufulize kukosa, magawio nayo yafurike? La, sivyo! Sisi tulioyafia makosa tutawezaje kuishi nayo tena?
Chunguza Waroma 6:1-2
8
Waroma 6:16
Hamjui, vilivyo? Ni hivi: mnapojitoa wenyewe kumtumikia mtu kitumwa na kumtii, basi, mmekwisha kuwa watumwa wake yeye, mnayemtii. Ikiwa ni wa ukosaji, mnakwenda kufa; ikiwa ni wa wito, mnakwenda kupata wongofu.
Chunguza Waroma 6:16
9
Waroma 6:17-18
Lakini Mungu atolewe shukrani, kwa sababu ninyi mliokuwa watumwa wa ukosaji mmegeuzwa mioyo, mkaja kuyatii mafundisho, kama mlivyoyapata! Napo hapo, mlipokombolewa katika utumwa wa ukosaji, mmegeuka kuwa watumwa wa wongofu.
Chunguza Waroma 6:17-18
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video