YouVersion Logo
Search Icon

Soma Biblia Kila Siku 02/2024Sample

Soma Biblia Kila Siku 02/2024

DAY 18 OF 29

Uhusiano kati ya Mungu na watu wake unagusa hali nzima ya maisha. Mungu anatakakukaa kati yao(m.8). Hivyo panahitajika mahali pa Mungu kukutania nao, na Waisraeli wamtolee Mungu vitu vyote vitakavyotumika kwa kumjengea nyumba. Lakini angalia ilivyoandikwa!Kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu(m.2). Atoe kwa hiari yake na kwa kadiri alivyofanikiwa. Tukumbuke pia kuwa matoleo haya yalitoka kwa Mungu:Wana wa Israeli wakafanya kama neno lile la Musa; wakataka kwa Wamisri vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu, na mavazi.Bwana akawajalia kupendelewa na Wamisri hata wakawapa kila walichokitaka. Nao wakawateka Wamisri nyara(Kut 12:35-36). Jihoji ukizingatia 1 Nya 29:17 na 2 Kor 9:7-8:Najua, Mungu wangu, ya kuwa wewe wajaribu moyo, nawe wapendezwa na unyofu. Nami katika unyofu wa moyo wangu nimeyatoa haya yote kwa hiari yangu mwenyewe; nami sasa nimeona kwa furaha watu wako, waliopo hapa, wakikutolea kwa hiari yao. …Kila mtu na atende kama alivyokusudia moyoni mwake, si kwa huzuni, wala si kwa lazima; maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo wa ukunjufu.Na Mungu aweza kuwajaza kila neema kwa wingi, ili ninyi, mkiwa na riziki za kila namna siku zote, mpate kuzidi sana katika kila tendo jema.

Scripture

About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 02/2024

Soma Biblia Kila Siku 02/ 2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Kutoka. Karibu kujiunga na mpango huu

More