Soma Biblia Kila Siku 06/2020Sample

Mtu akimwona ndugu yake anatenda dhambi isiyo ya mauti, ataomba (m.16). Mtume hakutofautisha ni dhambi zipi! Je, tunafanya nini tukimwona ndugu yetu akitenda dhambi? Je, tunamcheka? Hapa tunafundishwa kwamba inapotokea yatupasa kuomba. Kuna ahadi njema kwa maombi haya: Mungu atampa uzima. Dhambi iliyo ya mauti (m.16). Maana yake ni nini? Ni dhambi ya kumdharau Mungu na kuudharau wokovu aliotufanyia Yesu. Ni dhambi anayotenda mtu anapouharibu ule uhai aliopewa tayari na Mungu (linganisha na Yesu anavyoeleza Mt 12:32, Mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao). Inawezekana kuwa Yohana anapoandika kuhusu dhambi iliyo ya mauti, anafikiri juu ya hao waliotambulishwa katika barua hii kama wapinga Kristo (k.m. katika 2:22:Ni nani aliye mwongo ila yeye akanaye ya kuwa Yesu ni Kristo? Huyo ndiye mpinga Kristo).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 06/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 1 Yohana, Ayubu na Mathayo. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

God In The Times Of Kings

Breaking Busy: Find Peace & Purpose in the Crazy

Win the Day

Financial Discipleship – the Bible on Cosigning

Chosen for Love: A Journey With Jesus

Journey Through Kings & Chronicles Part 2

Walk With God: 3 Days of Pilgrimage

THE UPSIDE-DOWN KINGDOM: A 7 - Day Disovery of How God's Patterns for Living Turn Our Lives the Right Way Up by Youth Alive Aus

1 Corinthians
