Soma Biblia Kila Siku 6Sample

Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe (m.28). Mtumishi wa Bwana hapa ajifunze: 1.Asifikirie kulitunza kundi tu lakini pia akumbuke kujitunza nafsi yake! 2.Kwa njia gani atunze kundi na nafsi yake? a) Alishe kwa neno la neema (m.28: Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe; m.32: Nawaweka katika mikono ya Mungu, na kwa neno la neema yake, ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliotakaswa). b) Alinde(m.29-30 inatoa sababu: Mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi;tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao). c) Akeshe(m.31:kesheni, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana). d) Aonye(m.31: Sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi). e) Ajiweke mikononi mwa Mungu(m.32: Nawaweka katika mikono ya Mungu). f) Awasaidie wanyonge (m.35: Kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge). 3.Kanisa si lake Paulo (wala mtu mwingine yeyote), bali ni mali ya Yesu!
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Related Plans

Lead Through Prayer

Peace on Earth: A 5-Day Advent Devotional

Judges | Chapter Summaries + Study Questions

Let Us Pray

Returning Home: A Journey of Grace Through the Parable of the Prodigal Son

Stormproof

Homesick for Heaven

Faith in Hard Times

Breath & Blueprint: Your Creative Awakening
