1
Mathayo 7:7
Biblia Habari Njema
BHND
“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtapata; bisheni mlango, nanyi mtafunguliwa.
ប្រៀបធៀប
រុករក Mathayo 7:7
2
Mathayo 7:8
Maana, yeyote aombaye hupewa, atafutaye hupata, na abishaye mlango hufunguliwa.
រុករក Mathayo 7:8
3
Mathayo 7:24
“Kwa hiyo, kila mtu anayeyasikia maneno yangu na kuyazingatia, anafanana na mtu mwenye busara, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba.
រុករក Mathayo 7:24
4
Mathayo 7:12
“Yote mnayotaka watu wawatendee nyinyi, watendeeni wao vivyo hivyo. Hii ndiyo maana ya sheria ya Mose na mafundisho ya manabii.
រុករក Mathayo 7:12
5
Mathayo 7:14
Lakini njia inayoongoza kwenye uhai ni nyembamba, na mlango wa kuingilia humo ni mwembamba; ni watu wachache tu wanaoweza kuigundua njia hiyo.
រុករក Mathayo 7:14
6
Mathayo 7:13
“Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kwenye maangamizi ni pana, na mlango wa kuingilia humo ni mpana; waendao njia hiyo ni wengi.
រុករក Mathayo 7:13
7
Mathayo 7:11
Kama basi nyinyi, ingawa ni waovu, mwajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, hakika Baba yenu wa mbinguni atafanya zaidi: Atawapa mema wale wanaomwomba.
រុករក Mathayo 7:11
8
Mathayo 7:1-2
“Msiwahukumu wengine, msije nanyi mkahukumiwa na Mungu; kwa maana jinsi mnavyowahukumu wengine, ndivyo nanyi mtakavyohukumiwa; na kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho Mungu atakachotumia kwenu.
រុករក Mathayo 7:1-2
9
Mathayo 7:26
“Lakini yeyote anayesikia maneno yangu haya bila kuyazingatia, anafanana na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga.
រុករក Mathayo 7:26
10
Mathayo 7:3-4
Kwa nini wakiona kibanzi kilicho jichoni mwa ndugu yako, na papo hapo huioni boriti iliyoko jichoni mwako? Au, wawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi jichoni mwako,’ wakati wewe mwenyewe unayo boriti jichoni mwako?
រុករក Mathayo 7:3-4
11
Mathayo 7:15-16
“Jihadharini na manabii wa uongo. Wao huja kwenu wakionekana kama kondoo kwa nje, lakini kwa ndani ni mbwamwitu wakali. Mtawatambua kwa matendo yao. Je, watu huchuma zabibu katika miti ya miiba, au tini katika mbigili? La!
រុករក Mathayo 7:15-16
12
Mathayo 7:17
Basi, mti mzuri huzaa matunda mazuri, na mti mbaya huzaa matunda mabaya.
រុករក Mathayo 7:17
13
Mathayo 7:18
Mti mzuri hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mbaya hauwezi kuzaa matunda mazuri.
រុករក Mathayo 7:18
14
Mathayo 7:19
Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.
រុករក Mathayo 7:19
គេហ៍
ព្រះគម្ពីរ
គម្រោងអាន
វីដេអូ