Isaya 12
12
Wimbo wa shukrani
1Siku hiyo mutasema:
Ninakushukuru, ee Yawe,
maana ingawa ulinikasirikia,
hasira yako imetoweka,
nawe umenifariji.
2Mungu ndiye mwenye kuniokoa,
nitamutegemea yeye, wala sitaogopa;
Yawe ananijalia nguvu;
yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. #Ang. Kut 15.2; Zab 118.14
3Mutachota maji kwa furaha
kutoka visima vya wokovu.
4Siku hiyo mutasema:
Mumushukuru Yawe,
muombe kwa jina lake.
Mujulishe kwa mataifa matendo yake,
mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa.
5Mumwimbie Yawe sifa
maana ametenda mambo makubwa;
haya yajulikane katika dunia yote.
6Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha,
enyi wakaaji wa Sayuni,
maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.
Currently Selected:
Isaya 12: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.