YouVersion Logo
Search Icon

Isaya 12

12
Wimbo wa shukrani
1Siku hiyo mutasema:
Ninakushukuru, ee Yawe,
maana ingawa ulinikasirikia,
hasira yako imetoweka,
nawe umenifariji.
2Mungu ndiye mwenye kuniokoa,
nitamutegemea yeye, wala sitaogopa;
Yawe ananijalia nguvu;
yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. #Ang. Kut 15.2; Zab 118.14
3Mutachota maji kwa furaha
kutoka visima vya wokovu.
4Siku hiyo mutasema:
Mumushukuru Yawe,
muombe kwa jina lake.
Mujulishe kwa mataifa matendo yake,
mutangaze kuwa jina lake limetukuzwa.
5Mumwimbie Yawe sifa
maana ametenda mambo makubwa;
haya yajulikane katika dunia yote.
6Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha,
enyi wakaaji wa Sayuni,
maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.

Currently Selected:

Isaya 12: SWC02

Highlight

Copy

Compare

Share

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in