Isaya 13
13
Mungu ataazibu Babeli
1Haya ni maono, ambayo nabii Isaya mwana wa Amozi, aliyofunuliwa na Mungu juu ya inchi ya Babeli: #Ang. Isa 47.1-15; Yer 50.1–51.64
2Mungu anasema:
Musimike bendera juu ya mulima usiokuwa na miti,
muwapigie waaskari kelele,
muwapepee watu kwa mukono,
mukiwaita waingie kwenye milango ya muji wa wakubwa.
3Mimi nimewaamuru wachaguliwa wangu,
nimewaita mashujaa wangu,
hao wenye kunitukuza wakishangilia,
wakuje kutimiza hasira yangu.
4Musikilize kelele kwenye milima
kama za kundi kubwa la watu!
Musikilize kelele za falme,
na mataifa yanayokusanyika!
Yawe wa majeshi
analichunguza kundi linalokwenda kwa vita.
5Wanakuja kutoka inchi za mbali,
wanatoka hata miisho ya dunia:
Yawe na silaha za hasira yake
anakuja kuiangamiza dunia.
6Mulie, maana siku ya Yawe imekaribia;
inakuja kama uharibifu kutoka kwa Mungu Mwenye Nguvu. #Ang. Yoe 1.15
7Kwa hiyo mikono ya kila mutu itaregea,
kila mutu atavunjika moyo.
8Watu watafazaika,
watashikwa na hofu na maumivu,
watakuwa na uchungu kama mama anapozaa.
Wataangalia kwa mashaka,
nyuso zao zitaungua kwa haya.
9Siku ya Yawe inakuja,
siku kali, ya kasirani na hasira kali.
Itaifanya inchi kuwa uharibifu,
itawaangamiza wenye zambi ndani yake.
10Nyota na vikundi vyake katika anga hazitaangaza;
jua linapochomoza litakuwa giza,
na mwezi hautatoa mwangaza wake. #Ang. Eze 32.7; Mat 24.29; Mk 13.24-25; Lk 21.25; Ufu 6.12-13
11Yawe anasema hivi:
Nitauazibu ulimwengu kwa uovu wake,
waovu kwa sababu ya makosa yao.
Nitakikomesha kiburi cha wenye majivuno,
na kuporomosha mazarau ya watu wakali.
12Nitawafanya watu kuwa wachache kuliko zahabu safi;
wanadamu watakuwa wachache kuliko zahabu ya Ofiri.
13Nitazitetemesha mbingu
nayo inchi itatikisika katika misingi yake
kwa sababu ya kasirani ya Yawe wa majeshi,
siku ile ya hasira yangu kali.
14Kama swala anayewindwa,
kama kondoo wasiokuwa na muchungaji,
kila mumoja atajiunga na watu wake,
kila mutu atakimbilia katika inchi yake.
15Yeyote atakayeonekana atapigwa mukuki,
atakayekamatwa atauawa kwa upanga.
16Watoto wao wachanga watapondwapondwa mbele yao,
watanyanganywa nyumba zao,
na watalala na wake zao kwa kinguvu.
17Ninawachochea Wamedi juu yao;
watu ambao hawajali feza
wala hawavutwi na zahabu.
18Mishale yao itawaua vijana,
hawatarehemu watoto,
wala kuwahurumia watoto wachanga.
19Babeli ni utukufu wa falme zote
na sifa na majivuno ya Wakaldea
utakuwa kama Sodoma na Gomora,
wakati Mungu alipoiangamiza. #Ang. Mwa 19.24
20Hautakaliwa tena na watu hata kidogo,
watu hawataishi humo katika vizazi vyote.
Hakuna Mwarabu atakayesimamisha hema yake humo,
wala muchungaji atakayechunga nyama wake humo.
21Pahali pake ni nyama wakali wa pori ndio watakuwa ndani yake,
bundi watajaa katika nyumba zake.
Mbuni wataishi humo,
pepo watachezea huko. #Ang. Isa 34.14; Zef 2.14; Ufu 18.2
22Fisi watalia ndani ya pango zake,
mbweha wataonekana ndani ya nyumba zao za raha.
Wakati wa Babeli umekaribia,
wala siku zake hazitaongezwa.
Currently Selected:
Isaya 13: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.