YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 1

1
KITABU CHA KWANZA
(Zaburi 1–41)
Zaburi 1
Furaha Ya Kweli
1 Heri mtu yule ambaye
haendi katika shauri la watu waovu,
wala hasimami katika njia ya wenye dhambi,
au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 Bali huifurahia sheria ya Bwana,
naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa
kando ya vijito vya maji,
ambao huzaa matunda kwa majira yake
na majani yake hayanyauki.
Lolote afanyalo hufanikiwa.
Huzuni Ya Waovu
4 Sivyo walivyo waovu!
Wao ni kama makapi
yapeperushwayo na upepo.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,
wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki,
bali njia ya waovu itaangamia.

Currently Selected:

Zaburi 1: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy