YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 2

2
Zaburi 2
Mfalme Aliyechaguliwa Na Mungu
1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya,
na kabila za watu kula njama bure?
2 Wafalme wa dunia wanajipanga
na watawala wanajikusanya pamoja
dhidi ya Bwana
na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao
na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka,
Bwana huwadharau.
5 Kisha huwakemea katika hasira yake
na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 “Nimemtawaza Mfalme wangu
juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
Ushindi Wa Mfalme
7 Nitatangaza amri ya Bwana:
Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu,
leo mimi nimekuzaa.
8 Niombe, nami nitayafanya mataifa
kuwa urithi wako,
miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Utawatawala kwa fimbo ya chuma
na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima;
mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 Mtumikieni Bwana kwa hofu
na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Mbusu Mwana, asije akakasirika
nawe ukaangamizwa katika njia yako,
kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula.
Heri wote wanaomkimbilia.

Currently Selected:

Zaburi 2: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy