1
Mezali 3:5-6
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Umutumainie Yawe kwa moyo wako wote, wala usitegemee akili zako mwenyewe. Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.
Compare
Explore Mezali 3:5-6
2
Mezali 3:7
Usijione wewe mwenyewe kuwa mwenye hekima; umwogope Yawe na kujiepusha na uovu.
Explore Mezali 3:7
3
Mezali 3:9-10
Umuheshimu Yawe kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote. Kwa hiyo gala zako zitajaa ngano, na mitungi yako itafurika na divai mupya.
Explore Mezali 3:9-10
4
Mezali 3:3
Wema na uaminifu zisitengane nawe. Uvifunge katika shingo lako; uviandike ndani ya moyo wako.
Explore Mezali 3:3
5
Mezali 3:11-12
Mwana wangu, usizarau azabu ya Yawe, wala usiuzike kwa maonyo yake; maana Yawe anaonya yule anayemupenda, kama vile baba anavyomwonya mwana wake mupenzi.
Explore Mezali 3:11-12
6
Mezali 3:1-2
Mwana wangu, usisahau mafundisho yangu, lakini kwa moyo wako ushike amri zangu. Maana vitakupa wingi wa siku, maisha marefu na fanaka kwa wingi.
Explore Mezali 3:1-2
7
Mezali 3:13-15
Heri mutu anayetambua hekima, mutu yule anayepata ufahamu. Hekima ni bora kuliko feza, ina faida kuliko zahabu. Hekima ni ya maana sana kuliko mawe ya bei kali, hakuna kitu unachotamani kinachoweza kulingana nayo.
Explore Mezali 3:13-15
8
Mezali 3:27
Usimunyime mutu anayehitaji musaada, ikiwa una uwezo wa kufanya hivyo.
Explore Mezali 3:27
9
Mezali 3:19
Kwa hekima Yawe aliweka misingi ya dunia, kwa akili aliziimarisha mbingu.
Explore Mezali 3:19