1
Mezali 17:17
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Rafiki wa kweli ni rafiki siku zote. Ndugu anazaliwa kusudi asaidie wakati wa taabu.
Compare
Explore Mezali 17:17
2
Mezali 17:22
Moyo wenye furaha ni dawa, lakini moyo wenye huzuni unakondesha mwili.
Explore Mezali 17:22
3
Mezali 17:9
Anayesamehe makosa anajenga urafiki, lakini anayekumbusha makosa anatenga warafiki.
Explore Mezali 17:9
4
Mezali 17:27
Asiyesema sana ana maarifa; mutu mutulivu ni mwenye ufahamu.
Explore Mezali 17:27
5
Mezali 17:28
Hata mupumbafu akinyamaza, anaonekana kuwa na hekima; akifunga kinywa chake anaonekana kuwa mwenye akili.
Explore Mezali 17:28
6
Mezali 17:1
Afazali kula mukate wenye kukauka kwa amani kuliko karamu katika nyumba ya ugomvi.
Explore Mezali 17:1
7
Mezali 17:14
Kuanzisha ugomvi ni kama kufungua maji ya kisima; achana na ugomvi mbele haujafurika.
Explore Mezali 17:14
8
Mezali 17:15
Kumuhesabu mwovu kuwa na haki na kumwazibu asiyekuwa na kosa, yote mawili ni chukizo kwa Yawe.
Explore Mezali 17:15