1
Matayo 10:16
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.
Compare
Explore Matayo 10:16
2
Matayo 10:39
Kwa maana mutu anayetaka kulinda uzima wake, ataupoteza; lakini yule atakayetoa uzima wake kwa ajili yangu, ataupata tena.
Explore Matayo 10:39
3
Matayo 10:28
Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.
Explore Matayo 10:28
4
Matayo 10:38
Naye asiyejitolea kwa kubeba musalaba wake na kunifuata hastahili kuwa wangu.
Explore Matayo 10:38
5
Matayo 10:32-33
“Kila mutu anayenikubali mbele ya watu, nami nitamukubali vilevile mbele ya Baba yangu anayekuwa mbinguni. Lakini kila mutu anayenikana mbele ya watu, nami nitamukana vilevile mbele ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.
Explore Matayo 10:32-33
6
Matayo 10:8
Muponyeshe wagonjwa, mufufue wafu, mutakase wenye ukoma, mufukuze pepo. Mulipokea bure, mutoe bure vilevile.
Explore Matayo 10:8
7
Matayo 10:31
Basi musiogope, kwa sababu ninyi ni bora zaidi kuliko kundi la ndege wengi!
Explore Matayo 10:31
8
Matayo 10:34
“Musifikiri kwamba nimekuja kuleta amani katika dunia. Mimi sikukuja kuleta amani, lakini upanga.
Explore Matayo 10:34
Home
Bible
Plans
Videos