1
Muhubiri 3:1
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Kuna muda kwa kila kitu, na wakati kwa kila jambo katika dunia
Compare
Explore Muhubiri 3:1
2
Muhubiri 3:2-3
wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna kilichopandwa, wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga
Explore Muhubiri 3:2-3
3
Muhubiri 3:4-5
wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza, wakati wa kutupa mawe na wakati wa kukusanya mawe pamoja, wakati wa kukumbatia na wakati wa kutokumbatia
Explore Muhubiri 3:4-5
4
Muhubiri 3:7-8
wakati wa kupasua na wakati wa kushona, wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema, wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia, wakati wa vita na wakati wa amani.
Explore Muhubiri 3:7-8
5
Muhubiri 3:6
wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuchunga na wakati wa kutupa
Explore Muhubiri 3:6
6
Muhubiri 3:14
Ninajua kwamba jambo lolote Mungu analotenda linadumu milele. Hakuna kinachoweza kuongezwa wala kupunguzwa. Mungu amefanya mambo yakuwe hivyo kusudi wanadamu wamwogope yeye.
Explore Muhubiri 3:14
7
Muhubiri 3:17
Basi, nikasema ndani ya moyo wangu: “Mungu atawahukumu watu wa haki hata vilevile na waovu, maana amepanga wakati kwa kila jambo na kwa kila kazi.”
Explore Muhubiri 3:17