1
Muhubiri 2:26
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.
Compare
Explore Muhubiri 2:26
2
Muhubiri 2:24-25
Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu, maana usipojaliwa na Mungu, hauwezi kupata chakula wala kujifurahisha.
Explore Muhubiri 2:24-25
3
Muhubiri 2:11
Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.
Explore Muhubiri 2:11
4
Muhubiri 2:10
Kila kitu macho yangu yalichokitamani nilikipata. Moyo wangu sikuunyima raha yoyote. Moyo wangu ulifurahia mambo niliyotenda, na hii ilikuwa zawadi ya jasho langu.
Explore Muhubiri 2:10
5
Muhubiri 2:13
Basi, mimi nikagundua kwamba hekima ni bora kuliko upumbafu, kama vile mwangaza unavyokuwa bora kuliko giza.
Explore Muhubiri 2:13
6
Muhubiri 2:14
Mwenye hekima anaona anakokwenda, lakini mupumbafu anatembea katika giza. Hata hivyo, ninajua vilevile kwamba mwisho wao wote wawili ni mumoja.
Explore Muhubiri 2:14
7
Muhubiri 2:21
Maana, wakati mwingine, mutu ambaye amefanya kazi kwa kutumia hekima, akili na maarifa yake, anamwachia mutu mwingine afurahie matunda ya kazi ambayo hakuitoshea jasho. Hayo nayo ni bure. Ni jambo baya sana.
Explore Muhubiri 2:21