Soma Biblia Kila Siku 9Mfano

Kabla hajawa Mkristo, Paulo alielimika sana katika dini ya Kiyahudi. Kwa hiyo alijua maswali ya udadisi ambayo Wayahudi wangeweza kumwuliza kutokana na mafundisho yake. Kwa hiyo ameamua mwenyewe kuyauliza maswali haya na kuyajibu moja moja. Hii ni mbinu yake ya kuwafundisha Wakristo wa Rumi mambo ya msingi ya imani. Paulo anamlinganisha Myahudina Mtaifa akiuliza swali: Myahudi ana ziada gani? Na kutahiriwa kwafaa nini?(m.1). Sisitungeweza kumlinganishaMkristona Mtaifa na kujibu kama Paulo: Kwafaa sana kwa kila njia. Kwanza kwa kuwa wamekabidhiwa mausia ya Mungu(m.2). Zingatia pia kwamba kuasi kwa Myahudi (au Mkristo) hakumfanyi Mungu kuwa mwongo:Je! Kutokuamini kwao kutaubatili uaminifu wa Mungu?Hasha! Mungu aonekane kuwa amini na kila mtu mwongo(m.3-4)!
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 9 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kumbukumbu la Torati, Warumi na Mithali
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabolimo.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12

SOMA BIBLIA KILA SIKU 01/20

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Kusikia Kutoka Kwa Mungu Kila Asubuhi

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku 10

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021
