Soma Biblia Kila Siku 9Mfano

Basi, twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria (m.28). Njia ya kufika kwa Mungu ni moja kwa watu wote, nayo ni njia ya imani. Imani ya kuamini neema ya Mungu kwamba bila ustahili wangu ananisamehe dhambi zote kwa sababu ya upatanisho katika damu ya Yesu Kristo, ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake(m.25). Kwa kuamini haya twashinda katika kesi yetu mbele ya Mungu, yaani, twahesabiwa haki.Mungu ni hakimu na sisi ni washtakiwa. Twastahili hukumu ya kifo, lakini Mungu anatoa hukumu kuwa hatuna dhambi tunapomwamini Yesu, maana Yesu alipigwa na adhabu ya Mungu badala yetu!
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 9 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu na kupata maelezo mafupi ya kukusaidia kuendelea kutafakari na kuelewa Neno la Mungu. Mpango huu unagusa zaidi Kumbukumbu la Torati, Warumi na Mithali
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabolimo.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12

SOMA BIBLIA KILA SIKU 01/20

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Kusikia Kutoka Kwa Mungu Kila Asubuhi

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku 10

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021
