Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Uwekezaji Wako Ulio Bora!Mfano

Uwekezaji Wako Ulio Bora!

SIKU 3 YA 5

“Soma Biblia Mara kwa Mara”

Wengi wetu tutakubali kwamba Biblia imejaa mambo mengi   ya kusoma – baadhi yake yakionekana kutuzidi na hayaeleweki wakati mwingine.   Hapa ni kweli chache juu ya Biblia ambazo zitakusaidia unaposoma kuweza kufanya   rejea na kuelewa vizuri. 

Kwanza, utagundua kwamba Biblia imegawanyika katika   sehemu mbili: 

Agano la Kale ni mkusanyiko wa maandiko yanayoanzia na   uumbaji wa ulimwengu, historia ya watu wa Israeli – pamoja na kushindwa kwao   kama taifa, kuchukuliwa kwao mateka na maadui zao, na mwishoni kurudi kwao tena   na kuimiliki Yerusalemu mamia ya miaka michache kabla ya kuzaliwa kwa Kristo.   Agano la Kale pia ni sheria ya Mungu kwa Waisraeli. 

Agano Jipya ni mkusanyiko wa maandiko kuanzia muda  kidogo tu kabla kuzaliwa kwa Yesu, maisha na   huduma Yake, kifo Chake na kufufuka Kwake kama mwokozi, na pia kuanzishwa na   kupanuka kwa kanisa lake ulimwenguni pote. Ujumbe wa uhuru katika Kristo kwa   neema kama unavyofunuliwa katika Agano Jipya unatimiza na kufanyika mbadala   wa taratibu  zilizowekwa katika Agano   la Kale. 

Pili, na kwa kawaida, kuna aina tatu za maandiko   utakayoyaona katika Agano la Kale na Agano Jipya katika Biblia: 

Matukio ya Kihistoria - maandiko yanayoelezea simulizi za kweli na kutoa historia ya watu na   matukio muhimu. 

Maandiko yenye Maelekezo – vitabu na aya zinazotoa   maelekezo juu ya mambo mengi ya maisha ya Kikristo, utaratibu wa kanisa mambo   binafsi na mambo ya kifamilia bila kutoa mlolongo wa historia ya matukio.  

Maandiko yenye kuvutia -mashairi, maandiko ya kisanii yenye lengo la kutia moyo, kuinua na   kuonyesha hisia toka kwa mwandishi kwenda kwa msomaji. 

Maandiko ya Agano Jipya yanayotoa Matukio ya Kihistoria   ya maisha na huduma ya Yesu Kristo ni Mathayo, Marko, Luka na Yohana. Vitabu   hivi vinne pia vinaitwa Injili. Kitabu cha Matendo ya Mitume ni kitabu kingine   cha historia katika Agano Jipya ambacho kinabainisha kuanzishwa na kupanuka   kwa kanisa baada ya kifo cha Yesu na kufufuka kwake. 

Vitabu vya Agano Jipya vinavyohusisha Maandiko ya   Maelekezo ni Warumi mpaka Yuda. Hizi barua halisi kutoka viongozi wa kanisa   zikitoa ushauri na maelekezo kwa Wakristo wengine na makanisa ulimwenguni   pote. 

Kitabu cha Agano la Kale cha Zaburi ni mfano bora  wa maandiko yenye kuvutia. Hapa chini ni maandiko   yenye kuvutia kutoka Zaburi yanayotuhakikishia baraka ambazo Mungu humpatia   mtu ambaye huwekeza Neno la Mungu mara kwa mara katika maisha yake. 

“Bali   sheria ya BWANA ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na   usiku. Naye atakuwa kama mti uliopandwa kando kando ya vijito vya maji, Uzaao   matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo   litafanikiwa.” Zaburi 1:2-3

Kupanda   mbegu ya Neno la Mungu katika maisha yetu, tunahitaji kufanya usomaji wa   Biblia sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Pale mbegu ya Neno la Mungu   inaposhamiri katika maisha yako, baraka zake zitadhihirika zaidi. Utapokea   nguvu kutoka Neno Lake kukusaidia, hata katika wakati wa ukame na magumu.

Andiko

siku 2siku 4

Kuhusu Mpango huu

Uwekezaji Wako Ulio Bora!

Kupata matunda tele na ya baraka huanzia na kufanya uwekezaji ulio sahihi. Kama wewe ni mkristo mpya, hakuna uwekezaji ulio mkuu zaidi unaoweza kufanya katika imani yako zaidi ya kuingiza ndani yako Neno la Mungu mara k...

More

Tungependa kuwashukuru Twenty20 Faith, Inc. kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.twenty20faith.org/yvdev2

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha