Soma Biblia Kila Siku 5Mfano

Danieli aliheshimiwa kwa kuwa na roho bora ndani yake. Uaminifu wake kwa Mungu na watu ulimfanya awe safi. Ushuhuda na huduma yake ndivyo vilivyozua uadui baina yake na watumishi wa serikali. Kilipokosekana cha kumshtakia, basi wakamshtaki kwa sababu ya kutotii miungu yao. Lakini hata alipojua imani yake itamtia matatani, Danieli aliendelea kusali (m.10). Fundisho ni: Mungu ndiye anayetawala. Basi, kama Danieli, wewe usijali maadui, bali simamia kweli. Mungu atakulinda (Danieli alimwambia mfalme Dario, Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi nalionekana kuwa sina hatia; tena, mbele yako, Ee mfalme, sikukosa neno; Dan 6:22).
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 5 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku 8

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku 9

Soma Biblia Kila Siku 11

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku 10

Uamuzi Mkubwa Zaidi wa Maisha Yako!
