Methali 19:1-3
Methali 19:1-3 BHN
Afadhali maskini aishiye kwa unyofu, kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu. Haifai mtu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka hujikwaa. Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake, huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.