Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mithali 21:1-4

Mithali 21:1-4 NENO

Moyo wa mfalme uko katika mkono wa BWANA; huuongoza kama mkondo wa maji, popote apendapo. Njia zote za mwanadamu huonekana sawa kwake, bali BWANA huupima moyo. Kufanya yaliyo sawa na haki inakubalika zaidi kwa BWANA kuliko dhabihu. Macho ya kudharau na moyo wa kiburi, ambavyo ni taa ya waovu, vyote ni dhambi!