Kama vilivyokuwa siku za Noa, ndivyo kutakavyokuwa kurudi kwake Mwana wa mtu. Kwani siku zile zilizoyatangulia yale mafuriko makubwa ya maji walikuwa wakila, hata wakinywa, wakioa, hata wakiozwa mpaka siku, Nao alipoingia katika chombo kikubwa. Hawakuyatambua, mpaka mafuriko makubwa ya maji yakaja, yakawachukua wote pia. Ndivyo, kutakavyokuwa hata kurudi kwake mwana wa mtu.