Soma Biblia Kila Siku 05/2024Sample

Watanzania wengi wametolewa mapepo kwa jina la Yesu. Kwa hiyo tunahitaji kuwa makini sana kuyaangalia mafundisho ya Yesu katika m.43-45:Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate. Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa. Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya! Hapa Yesu anatuonyesha umuhimu wa kumtunza kiroho mtu wa namna hiyo. Huduma yetu haina maana, ikiwa mtu amesaidiwa kwa siku moja, wiki moja au mwaka mmoja tu. Asiposaidiwa kiasi cha kuweza kusimama imara katika Yesu na kufika Mbinguni, hatujafanikiwa huduma yetu. Kuna utupu katika moyo wa mtu baada ya kutolewa pepo. Ni lazima utupu huu ujazwe na neno la Mungu na sala!
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 05/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa tano pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Kutoka, Yoeli na Mathayo. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

The Cross: Why Did Jesus Have to Die?

God's Love Letter to You - Chronological Bible in a Year

Daily Godpreneur: Millionaire Mind

Faith in Trials!

No Days Off: A 7-Day Devotional

The Biscuit Trail

Rain Devotional: A 3-Day Journey of Restoration, Revival, and Redirection

Soulcon Warrior 7 Day Devotional

Colossians & Philemon Book Study - TheStory
