Soma Biblia Kila Siku 05/2024Sample

Yesu anafundisha juu ya jambo moja ambalo kwa kawaida hukosekana kwa sisi wanadamu, yaaniunyenyekevu wa moyo mbele ya Mungu. Bila unyenyekevu huu hatuwezi kumtambua Mungu wala Mwana wake, Yesu Kristo. Yesu hujiweka mwenyewe kuwa mfano kwetu katika hili. Katika m.29 anasema:Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu. Ni jambo hili Paulo anakumbusha katika Flp 2:5-8, akiandika:Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye ... alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.Watoto wachanga pia ni mfano, maana wanahitaji kupokea kila kitu na wala hawawezi kuijisifia uwezo wowote. Katika m.25 Yesu anamwambia Mungu:Mambo hayauliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Basi, sikia wito wa Yesu katika m.28:Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha;ukajinyenyekeze mbele yake! Hivyoutapata raha nafsini mwako(m.29).
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku 05/2024 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu kwa mwezi wa tano pamoja na maelezo mafupi ya kukusaidia kutafakari somo ulilosoma. Katika mpango huu utasoma zaidi kitabu cha Kutoka, Yoeli na Mathayo. Karibu kujiunga na mpango huu
More
Related Plans

Awakening Faith: Hope From the Global Church

Game Changers: Devotions for Families Who Play Different (Age 8-12)

30 Powerful Prayers for Your Child Every Day This School Year

Sharing Your Faith in the Workplace

Rebuilt Faith

Protocols, Postures and Power of Thanksgiving

24 Days to Reflect on God's Heart for Redemption

Legacy Lessons W/Vance K. Jackson

You Say You Believe, but Do You Obey?
