Soma Biblia Kila Siku Disemba/2022Sample

Kama alivyoanza katika m.13, Daudi anahitimisha zaburi hii kwa maneno ya sifa. Jambo kuu ni kumshukuru Mungu kwa jinsi alivyompigania. Daudi alimtegemea Mungu kama mwamba na wokovu wake (m.46, Ahimidiwe mwamba wangu; na atukuzwe Mungu wa wokovu wangu). Kwa hiyo alijikabidhi kwake katika hali zote. Hata sasa baada ya kuinuliwa juu sana, Daudi anaendelea kumtegemea Mungu. Katika m.50b anasema, Amfanyia fadhili masihi wake, Daudi na mzao wake hata milele. Hapo anaonyesha imani yake katika ahadi ya Mungu kwa Daudi, kama tunavyoisoma katika 2 Sam 7:16: Na nyumba yako, na ufalme wako, vitathibitishwa milele mbele yako. Nacho kiti chako kitafanywa imara milele. Angalia kuwa kwa njia hiyo habari ya wokovu wa Mungu iliwafikia hata watu wa mataifa (m.49, BWANA, nitakushukuru kati ya mataifa), na mfalme Daudi alipata kuwa mfano wa Masihi, yaani, Kristo Yesu.
Scripture
About this Plan

Soma Biblia Kila Siku Disemba/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Disemba pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa siku husika. Katika mpango huu utasoma zaidi katika kitabu cha Luka na Zaburi. Karibu kujiunga na mpango huu na usome bure
More
Related Plans

FruitFULL - Faithfulness, Gentleness, and Self-Control - the Mature Expression of Faith

Peace in Chaos for Families: 3 Days to Resilient Faith

Daniel in the Lions’ Den – 3-Day Devotional for Families

The Bible, Simplified

Spring of Renewal

Connect

Rich Dad, Poor Son

What Is My Calling?

Beautifully Blended | Devotions for Couples
