Injili Ulimwenguni - Sehemu 2Sample

Yesu aponia mwana wa afia wa kifalme
Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya. (Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.)
Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria kwenye hiyo Sikukuu. Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai.
"Huko kulikuwako na mtu mmoja afisa wa kifalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu.
Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.
“Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”
“Bwana, Yule afisa wa kifalme akamwambia, "tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”
Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.”
Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake.
"Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima.
Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”
Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye, pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.
Scripture
About this Plan

Mfuatano huu ni kusanyiko la hadithi kuhusu maisha Kristo itakayoshirikisha watazamaji wote ulimwenguni kwa kutumia mchanganyiko wa kuona na sauti. Maisha na mafundisho ya Yesu yalidhihirishwa katika kitabu hiki cha hadithi ambacho kinafuata masimulizi ya Agano Jipya yanayopatikana katika vitabu vya Injili vya Mathayo, Marko, Luka, na Yohana.
More
Related Plans

Transformational Days of Courage for Women

Faith in Hard Times

God’s Answer to Anxiety: 7 Truths That Calm the Chaos Inside

Unapologetically Sold Out: 7 Days of Prayers for Millennials to Live Whole-Heartedly Committed to Jesus Christ

God Says I Am: Embracing Peace & Walking in Power

The Book of Psalms (30-Day Journey)

When You’re Desperate: 21 Days of Honest Prayer

Lost Kings | Steward Like a King

Breath & Blueprint: Your Creative Awakening
