YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 36

36
Uovu wa binadamu
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi, mtumishi wa Mwenyezi-Mungu)
1 # Taz Rom 3:18 Dhambi huongea na mtu mwovu,
ndani kabisa moyoni mwake;
jambo la kumcha Mungu halimo kabisa kwake.
2Mwovu hujipendelea mwenyewe,
hufikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.
3Kila asemacho ni uovu na uongo;
ameacha kutumia hekima na kutenda mema.
4Alalapo huwaza kutenda maovu,
hujiweka katika njia isiyo njema,
wala haachani na uovu.
Wema wa Mungu
5Fadhili zako ee Mwenyezi-Mungu zaenea hata mbinguni;
uaminifu wako wafika mawinguni.
6Uadilifu wako ni kama milima mikubwa,
hukumu zako ni kama vilindi vya bahari.
Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, wawalinda wanadamu na wanyama
7Jinsi gani zilivyo bora fadhili zako!
Wanadamu hukimbilia kivulini mwa mabawa yako.
8Wawashibisha kwa utajiri wa nyumba yako;
wawanywesha kutoka mto wa wema wako.
9Wewe ndiwe asili ya uhai;
kwa mwanga wako twaona mwanga.
10Uendelee kuwafadhili wale wanaokutambua;
uzidi kuwa mwema kwa wanyofu wa moyo.
11Usikubali wenye majivuno wanivamie,
wala watu waovu wanikimbize.
12Kumbe watendao maovu wameanguka;
wameangushwa chini, hawawezi kuinuka.

Currently Selected:

Zaburi 36: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy