YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 25

25
Kumwomba Mungu uongozi na ulinzi
(Zaburi ya Daudi)
1Ee Mwenyezi-Mungu, kwako naielekeza nafsi yangu!
2Nakutumainia wewe, ee Mungu wangu,
usiniache niaibike;
adui zangu wasifurahie kushindwa kwangu.
3Usimwache anayekutumainia apate aibu;
lakini waaibike wote wanaokuasi kwa makusudi.
4Unijulishe njia zako, ee Mwenyezi-Mungu;
unifundishe nifuate unayotaka.
5Uniongoze katika ukweli wako na kunifundisha,
kwani wewe ni Mungu, mwokozi wangu;
ninakutegemea wewe kila siku.
6Uikumbuke huruma yako ee Mwenyezi-Mungu;
uzikumbuke na fadhili zako kuu,
ambazo zimekuwako tangu kale.
7Usikumbuke dhambi na makosa ya ujana wangu;
unikumbuke kadiri ya fadhili zako,
kwa ajili ya wema wako, ee Mwenyezi-Mungu.
8Mwenyezi-Mungu ni mwema na mnyofu,
kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia.
9Huwaongoza wanyenyekevu katika uadilifu;
naam, huwafundisha hao njia yake.
10Mwenyezi-Mungu hutenda kwa fadhili na uaminifu,
kwa wale wanaoshika agano lake na maamuzi yake.
11Kwa ajili ya jina lako, ee Mwenyezi-Mungu,
unisamehe kosa langu kwani ni kubwa.
12Kila mtu anayemcha Mwenyezi-Mungu,
Mwenyezi-Mungu atamfunza njia ya kufuata.
13Mtu wa namna hiyo atafanikiwa daima,
na wazawa wake watamiliki nchi.
14Mwenyezi-Mungu ni rafiki ya wale wamchao;
yeye huwajulisha hao agano lake.
15Namwangalia Mwenyezi-Mungu daima;
yeye atainasua miguu yangu mtegoni.
16Unielekee, ee Mungu, unionee huruma,
maana mimi ni mpweke na mnyonge.
17Uniondolee mahangaiko ya moyoni mwangu;
unitoe katika mashaka yangu.
18Uangalie mateso yangu na dhiki yangu;
unisamehe dhambi zangu zote.
19Angalia jinsi walivyo wengi maadui zangu;
ona jinsi wanavyonichukia kwa ukatili.
20Uyalinde maisha yangu, uniokoe;
nakimbilia usalama kwako,
usikubali niaibike.
21Wema na uadilifu vinihifadhi,
maana ninakutumainia wewe.
22Ee Mungu, uwaokoe watu wako, Israeli;
uwaokoe katika taabu zao zote.

Currently Selected:

Zaburi 25: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy