YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 20

20
Kuomba ushindi
(Kwa Mwimbishaji. Zaburi ya Daudi)
1Mwenyezi-Mungu akujibu uwapo taabuni;
jina la Mungu wa Yakobo likulinde.
2Akupelekee msaada kutoka hekaluni mwake;
akutegemeze kutoka mlima Siyoni.
3Azikumbuke sadaka zako zote;
azikubali tambiko zako za kuteketezwa.
4Akujalie unayotamani moyoni mwako,
aifanikishe mipango yako yote.
5Tutashangilia kwa ajili ya ushindi wako;
tutatweka bendera kulitukuza jina la Mungu wetu.
Mwenyezi-Mungu akutimizie maombi yako yote!
6Najua Mwenyezi-Mungu atamsaidia mfalme aliyemteua,
atamjibu kutoka patakatifu pake mbinguni;
kwa mkono wake wa kulia atamjalia ushindi mkubwa.
7Wengine hujigamba kwa magari ya vita;
wengine hujigamba kwa farasi wao.
Lakini sisi twajivunia Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.
8Hao watajikwaa na kuanguka;
lakini sisi tutainuka na kusimama imara.
9Umjalie mfalme ushindi, ee Mwenyezi-Mungu;
utujibu wakati tunapokuomba.

Currently Selected:

Zaburi 20: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy