Malaki 2
2
1Mwenyezi-Mungu wa majeshi awaambia makuhani: “Sasa enyi makuhani, nawaamuruni hivi: 2Ni lazima mniheshimu mimi kwa matendo yenu, msiponisikiliza nitawaleteeni laana, vitu vyote mnavyopewa kwa mahitaji yenu nitavilaani. Na kweli nimekwisha kuvilaani, kwa sababu hamuyatilii maanani maagizo yangu. 3Tazama, nitawaadhibu watoto wenu na nyinyi wenyewe kutokana na uovu wenu, na kuzipaka nyuso zenu mavi ya wanyama wenu wa tambiko. Nitawafukuza mbali nami. 4#Taz Hes 3:11-13 Hivyo mtajua kuwa nimewapeni amri hii ili agano langu na ukoo wa Lawi liwe la kudumu.
5 # Taz Hes 25:12 “Katika agano hilo, niliwaahidi uhai na amani na kwamba wao ni lazima kunicha mimi, nao kwa upande wao walinicha mimi, wakaliogopa jina langu. 6Mafundisho yao yalikuwa ya kweli na kamwe hawakufundisha uongo. Mimi na wao tulikaa kwa amani. Si kwamba walitenda haki tu, bali waliwafundisha wengine kutotenda maovu. 7Ni wajibu wa makuhani kuwafundisha watu maarifa ya kweli juu ya Mungu. Watu wawaendee kujifunza matakwa yangu kwao, kwani makuhani ni wajumbe wa Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
8“Bali nyinyi makuhani mmegeuka mkaiacha njia ya haki. Mafundisho yenu yamewaongoza watu wengi katika kutenda mabaya. Mmelivunja agano nililofanya nanyi. 9Nami pia nitawafanya mdharauliwe na kupuuzwa na Waisraeli, kwa sababu hamkuzifuata njia zangu, na mnapowafundisha watu wangu mnapendelea baadhi yao.”
Watu si waaminifu kwa Mungu
10Je, sisi sote si watoto wa baba mmoja? Je, sisi sote hatukuumbwa na Mungu yuleyule? Mbona basi, hatuaminiani sisi kwa sisi, na tunalidharau agano alilofanya Mwenyezi-Mungu na wazee wetu? 11Watu wa Yuda wamekosa uaminifu kwa Mungu na kutenda machukizo katika Israeli na mjini Yerusalemu. Wamelitia unajisi hekalu la Mwenyezi-Mungu analolipenda. Tena wameoa wanawake wanaoabudu miungu ya kigeni. 12Mwenyezi-Mungu na awaondolee mbali watu wanaofanya mambo hayo kutoka miongoni mwa wazawa wa Yakobo. Na kamwe wasishiriki katika kutoa ushuhuda na kuleta tambiko mbele ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi.
13Zaidi ya hayo yote, mnaifunika madhabahu ya Mwenyezi-Mungu kwa machozi yenu, mkilia na kuomboleza kwa sababu yeye hazikubali tena tambiko mnazomtolea. 14Mnauliza, “Mbona sasa hazikubali?” Mwenyezi-Mungu hazikubali kwa sababu anajua wazi kuwa umeivunja ahadi yako kwa mke wa ujana wako. Umekosa uaminifu kwake ingawa uliahidi mbele ya Mungu kwamba ungekuwa mwaminifu kwake. 15Je, Mungu hakuwafanya nyote wawili muwe mwili mmoja na roho moja?#2:15 Je … moja: Maana katika Kiebrania si dhahiri. Je, alikusudia nini alipofanya hayo? Yamkini alikusudia tuzae watoto ambao watamcha yeye. Kwa hiyo, hakikisheni kuwa hakuna hata mmoja wenu anayekosa uaminifu kwa mkewe. 16Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema: “Ninachukia talaka. Ninachukia mmoja wenu anapomtendea mkewe ukatili huo. Hakikisheni kwamba hakuna hata mmoja wenu anayekosa uaminifu kwa mkewe.”
Siku ya hukumu i karibu
17Mmemchosha Mwenyezi-Mungu kwa maneno yenu matupu. Hata hivyo, mnasema, “Tumemchoshaje?” Mmemchosha mnaposema, “Mwenyezi-Mungu huwaona kuwa wema watu wanaotenda maovu; tena anawapenda.” Au mnapouliza, “Yuko wapi yule Mungu mwenye haki?”
Currently Selected:
Malaki 2: BHN
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Malachi 2
2
Corrupt Priests
1“And now, O #Mal. 1:6priests, this commandment is for you.
2#(Lev. 26:14, 15; Deut. 28:15)If you will not hear,
And if you will not take it to heart,
To give glory to My name,”
Says the Lord of hosts,
“I will send a curse upon you,
And I will curse your blessings.
Yes, I have cursed them #Mal. 3:9already,
Because you do not take it to heart.
3“Behold, I will rebuke your descendants
And spread #Ex. 29:14refuse on your faces,
The refuse of your solemn feasts;
And one will #1 Kin. 14:10take you away with it.
4Then you shall know that I have sent this commandment to you,
That My covenant with Levi may continue,”
Says the Lord of hosts.
5“My#Num. 25:12; Ezek. 34:25 covenant was with him, one of life and peace,
And I gave them to him #Deut. 33:9that he might fear Me;
So he feared Me
And was reverent before My name.
6#Deut. 33:10The law of truth was in his mouth,
And injustice was not found on his lips.
He walked with Me in peace and equity,
And #Jer. 23:22; (James 5:20)turned many away from iniquity.
7“For#Num. 27:21; Deut. 17:8–11; Jer. 18:18 the lips of a priest should keep knowledge,
And people should seek the law from his mouth;
#(Gal. 4:14)For he is the messenger of the Lord of hosts.
8But you have departed from the way;
You #Jer. 18:15have caused many to stumble at the law.
#Num. 25:12, 13; Neh. 13:29; Ezek. 44:10You have corrupted the covenant of Levi,”
Says the Lord of hosts.
9“Therefore #1 Sam. 2:30I also have made you contemptible and base
Before all the people,
Because you have not kept My ways
But have shown #Deut. 1:17; Mic. 3:11; 1 Tim. 5:21partiality in the law.”
Treachery of Infidelity
10#Jer. 31:9; 1 Cor. 8:6; (Eph. 4:6)Have we not all one Father?
#Job 31:15Has not one God created us?
Why do we deal treacherously with one another
By profaning the covenant of the fathers?
11Judah has dealt treacherously,
And an abomination has been committed in Israel and in Jerusalem,
For Judah has #Ezra 9:1, 2; Neh. 13:23profaned
The Lord’s holy institution which He loves:
He has married the daughter of a foreign god.
12May the Lord cut off from the tents of Jacob
The man who does this, being awake and aware,
Yet #Neh. 13:29who brings an offering to the Lord of hosts!
13And this is the second thing you do:
You cover the altar of the Lord with tears,
With weeping and crying;
So He does not regard the offering anymore,
Nor receive it with goodwill from your hands.
14Yet you say, “For what reason?”
Because the Lord has been witness
Between you and #Prov. 5:18; Jer. 9:2; Mal. 3:5the wife of your youth,
With whom you have dealt treacherously;
#Prov. 2:17Yet she is your companion
And your wife by covenant.
15But #Gen. 2:24; Matt. 19:4, 5did He not make them one,
Having a remnant of the Spirit?
And why one?
He seeks #Ezra 9:2; (1 Cor. 7:14)godly offspring.
Therefore take heed to your spirit,
And let none deal treacherously with the wife of his youth.
16“For #Deut. 24:1; (Matt. 5:31; 19:6–8)the Lord God of Israel says
That He hates divorce,
For it covers one’s garment with violence,”
Says the Lord of hosts.
“Therefore take heed to your spirit,
That you do not deal treacherously.”
17#Is. 43:22, 24You have wearied the Lord with your words;
Yet you say,
“In what way have we wearied Him?”
In that you say,
#Is. 5:20; Zeph. 1:12“Everyone who does evil
Is good in the sight of the Lord,
And He delights in them,”
Or, “Where is the God of justice?”
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
The Holy Bible, New King James Version, Copyright © 1982 Thomas Nelson. All rights reserved.