Zaburi 52
52
Hukumu ya Mungu
1-2Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Daudi yanayoelekea wakati Doegi wa Edomu alipomwendea Saulo na kumujulisha kwamba Daudi amemwendea Ahimeleki.
3Mbona, ewe jitu,
unajivunia mabaya unayotendea waaminifu.
4Kila wakati unawaza maangamizi.
Ulimi wako ni kama wembe mukali.
Unafikiria tu kutenda mabaya.
5Wewe unapenda ubaya kuliko uzuri,
unapenda uongo kuliko ukweli.
6Ewe mudanganyifu mukubwa,
unapenda mambo ya kuangamiza wengine.
7Kwa hiyo Mungu atakuangamiza milele,
atakunyanyua na kukuondoa katika nyumba yako;
atakuongoa katika inchi ya wenye kuishi.
8Watu wa haki wataona, wataogopa,
na kisha watakuchekelea na kusema:
9“Muangalie yaliyomupata mutu huyu!
Yeye hakutaka Mungu akuwe kimbilio lake,
lakini alitegemea wingi wa mali yake,
na kutafuta humo usalama wake!”
10Lakini mimi ni kama muzeituni mubichi,
unaostawi katika nyumba ya Mungu.
Ninategemea wema wake milele na milele.
11Ee Mungu, nitakushukuru siku zote,
kwa ajili ya mambo uliyofanya.
Nitatangaza kwamba wewe ni muzuri,
mbele ya watu wako waaminifu.
Currently Selected:
Zaburi 52: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.
Zaburi 52
52
Hukumu ya Mungu
1-2Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Daudi yanayoelekea wakati Doegi wa Edomu alipomwendea Saulo na kumujulisha kwamba Daudi amemwendea Ahimeleki.
3Mbona, ewe jitu,
unajivunia mabaya unayotendea waaminifu.
4Kila wakati unawaza maangamizi.
Ulimi wako ni kama wembe mukali.
Unafikiria tu kutenda mabaya.
5Wewe unapenda ubaya kuliko uzuri,
unapenda uongo kuliko ukweli.
6Ewe mudanganyifu mukubwa,
unapenda mambo ya kuangamiza wengine.
7Kwa hiyo Mungu atakuangamiza milele,
atakunyanyua na kukuondoa katika nyumba yako;
atakuongoa katika inchi ya wenye kuishi.
8Watu wa haki wataona, wataogopa,
na kisha watakuchekelea na kusema:
9“Muangalie yaliyomupata mutu huyu!
Yeye hakutaka Mungu akuwe kimbilio lake,
lakini alitegemea wingi wa mali yake,
na kutafuta humo usalama wake!”
10Lakini mimi ni kama muzeituni mubichi,
unaostawi katika nyumba ya Mungu.
Ninategemea wema wake milele na milele.
11Ee Mungu, nitakushukuru siku zote,
kwa ajili ya mambo uliyofanya.
Nitatangaza kwamba wewe ni muzuri,
mbele ya watu wako waaminifu.
Currently Selected:
:
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.