Zaburi 46
46
Mungu yuko upande wetu
1Kwa mukubwa wa waimbaji. Zaburi ya Wakora: Kwa mutindo wa Sauti ya juu kabisa.
2Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu;
yeye ni musaada wetu wakati wa taabu.
3Kwa hiyo hatutaogopa kitu chochote,
hata dunia ikiyeyuka
na milima kutikisika kutoka bahari,
4hata kama bahari ikichafuka na kutisha,
na milima ikitetemeka kwa machafuko yake.
5Kuna muto ambao maji yake yanafurahisha muji wa Mungu,
makao matakatifu ya Mungu Mukubwa.
6Mungu yuko katika muji huo, nao hauwezi kutikiswa;
Mungu ataupatia musaada kila asubui.
7Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika;
Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.
8Yawe wa majeshi yuko pamoja nasi,
Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.
9Mukuje muone matendo ya Yawe.
Muone maajabu aliyofanya katika dunia.
10Anakomesha vita popote katika dunia.
Anavunjavunja pinde na mikuki,
nayo magari ya vita anayateketeza.
11Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu!
Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote;
mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”
12Yawe wa majeshi yuko pamoja nasi,
Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu.
Currently Selected:
Zaburi 46: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.