Hesabu 27
27
Haki ya kurizi kwa wanawake
1Mala, Noa, Hogla, Milka na Tirsa walikuwa wabinti za Selofehadi. Naye Selofehadi alikuwa mwana wa Heferi mwana wa Gileadi mwana wa Makiri mwana wa Manase mwana wa Yosefu. 2Basi, hao wabinti wane wakamwendea Musa, wakasimama mbele yake na kuhani Eleazari na viongozi wote wa Waisraeli, kwenye mulango wa hema la mukutano, wakasema: 3Baba yetu alikufia katika jangwa na bila mutoto yeyote mwanaume. Yeye hakukuwa kati ya wafuasi wa Kora waliokusanyika mbele ya Yawe, lakini alikufa kutokana na zambi yake mwenyewe. Hakukuwa na mutoto mwanaume. 4Kwa nini basi jina la baba yetu lifutwe katika ukoo wake kwa sababu hakukuwa na mutoto mwanaume? Utupatie urizi pamoja na wandugu za baba yetu.
5Musa akaleta malalamiko yao mbele ya Yawe. 6Yawe akamwambia Musa: 7Wanachosema wabinti za Selofehadi ni kweli; uwape urizi pamoja na wandugu za baba yao, watwae urizi wake. #Ang. Hes 36.2 8Kisha uwaambie Waisraeli kwamba mutu yeyote akikufa bila kuacha mutoto mwanaume, urizi wake utapewa kwa binti yake. 9Ikiwa hana binti, basi urizi huo utapewa kwa wandugu zake wanaume. 10Na ikiwa hana ndugu mwanaume, basi urizi wake utawaendea baba zake wakubwa na wadogo. 11Na ikiwa baba yake hana ndugu mwanaume, basi urizi wake utamwendea wandugu zake wa karibu, naye ataurizi kama vile mali yake. Hii itakuwa sharti na agizo kwa Waisraeli, kama vile mimi Yawe nilivyokuamuru.
Yoshua anachaguliwa kuwaongoza Waisraeli
(Kumb 31.1-8)
12Yawe akamwambia Musa: Panda juu ya mulima huu wa miinuko ya Abarimu uangalie inchi ambayo nimewapa Waisraeli. #Ang. Kumb 3.23-27; 32.48-52 13Ukisha kuiona, utakufa na kukutana na wazee wako, kama vile ndugu yako Haruni alivyokutana nao, 14kwa sababu hamukuitii amri yangu kule katika jangwa la Sini, wakati watu wote pamoja waliponigombanisha kule Meriba. Ninyi hamukuacha utukufu wangu uonekane mbele yao walipotaka wapewe maji. (Meriba ni chemichemi ya maji ya Kadesi katika jangwa la Sini).
15Naye Musa akamwomba Yawe: 16Ee Yawe, Mungu unayekuwa asili ya uzima wote, ninakuomba umuchague mutu wa kusimamia watu hawa, 17ambaye atawatangulia na kuwaongoza katika shuguli zao zote, kusudi wasikuwe kama kondoo wasiokuwa na muchungaji. #Ang. 1 Fal 22.17; Eze 34.5; Mat 9.36; Mk 6.34
18Yawe akamwambia Musa: Umutwae Yoshua mwana wa Nuni, mutu mwenye roho nzuri, kisha uweke mikono juu yake, #Ang. Kut 24.13 19na kumusimamisha mbele ya kuhani Eleazari na watu wote, umupatie kazi hiyo. 20Umupe sehemu ya mamlaka yako kusudi Waisraeli wote wamutii. 21Yeye atamutegemea kuhani Eleazari ambaye atamujulisha mapenzi yangu kwa kutumia jiwe la shauri.#27.21 jiwe la shauri: Kiebrania: “Urimu”: moja ya mawe mawili yaliyotumiwa na kuhani kujua mapenzi ya Mungu. Kwa njia hii, Eleazari atamwongoza Yoshua na Waisraeli wote wanapotoka na wanapoingia. #Ang. Kut 28.30; 1 Sam 14.41; 28.6 22Musa akafanya kama vile alivyoamriwa na Yawe. Akamutwaa Yoshua na kumusimamisha mbele ya kuhani Eleazari na Waisraeli wote. 23Kisha akamwekea mikono juu ya kichwa na kumupa mamlaka kama vile alivyoagizwa na Yawe. #Ang. Kumb 31.23
Currently Selected:
Hesabu 27: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.