YouVersion Logo
Search Icon

Walawi 24

24
Taa za Pahali Patakatifu
(Kut 27.20-21)
1Yawe akamwambia Musa: 2Uwaamuru watu wa Israeli wakuletee mafuta safi kwa ajili ya taa kusudi taa hiyo iendelee kuwaka siku zote. 3Haruni ataweka taa hiyo ndani ya hema la mukutano, inje ya pazia la Sanduku la Agano kusudi ipate kuwaka mbele yangu tangu usiku mpaka asubui. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyenu. 4Ataweka hizo taa katika kinara cha taa cha zahabu safi ziwake siku zote mbele ya Yawe.
5Twaa unga laini, kilo kumi na mbili na kupika mikate kumi na miwili. #Ang. Kut 25.30 6Mikate hiyo itapangwa kwa mistari miwili juu ya meza ya zahabu safi, kila mustari mikate sita. 7Kila mustari utautia ubani safi kusudi uambatane na mikate hiyo na kuwa sehemu ya sadaka ya kuteketezwa ya ukumbusho kwa Yawe. 8Kila siku ya Sabato Haruni ataipanga sawasawa katika mustari mbele yangu mimi Yawe kwa ajili ya watu wa Israeli kama vile agano la milele. 9Haruni na wazao wake peke yao ndio wanaoruhusiwa kula mikate hiyo maana ni mitakatifu kabisa kwa sababu ni sehemu ya sadaka ninazotolewa mimi Yawe kwa moto. Hiyo ni haki yao milele. #Ang. Mat 12.4; Mk 2.26; Lk 6.4
Azabu ya haki
10Siku moja kukatokea fujo kule katika kambi kati ya Mwisraeli mumoja na kijana mumoja wa mama Mwisraeli lakini baba Mumisri. 11Yule kijana ambaye mama yake aliitwa Selemoti binti ya Dibri wa kabila la Dani, alitukana Mungu na kuzarau jina lake. Basi watu wakamupeleka kijana kwa Musa, 12wakamutia katika kifungo mpaka pale watakapofunuliwa mapenzi ya Yawe.
13Basi, Yawe akamwambia Musa: 14Umuondoe kijana aliyetukana inje ya kambi, wale wote waliomusikia akitukana waweke mikono yao juu ya kichwa chake, na wote pamoja wamwue kwa kumupiga mawe. 15Nawe uwaambie Waisraeli kwamba mutu yeyote atakayemulaani Mungu wake atabeba lazima ya zambi yake. 16Mutu yeyote akuwe ni mwenyeji au mugeni anayemutukana Yawe, wote pamoja watamwua kwa kumupiga mawe. 17Mutu yeyote anayeua mutu mwingine anapaswa naye kuuawa. #Ang. Kut 21.12 18Mutu yeyote anayeua nyama wa mwenzake anapaswa kutoa malipo: uzima kwa uzima. 19Mutu yeyote anayemwumiza mwenzake, anapaswa naye aumizwe sawasawa na vile alivyomwumiza mwenzake, 20akimuvunja mufupa naye atavunjwa mufupa, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kila mutu anayemwumiza mwenzake anapaswa naye aumizwe kulingana na tendo lake. #Ang. Kut 21.23-25; Kumb 19.21; Mat 5.38 21Anayemwua nyama anapaswa kutoa malipo, lakini mutu yeyote akimwua mutu mwingine anapaswa naye auawe. 22Sheria hii inaelekea mugeni na mwenyeji. Mimi ni Yawe, Mungu wenu. #Ang. Hes 15.16
23Basi, Musa akawaambia Waisraeli hayo yote. Wakamupeleka yule mutu aliyelaani Yawe inje ya kambi, wakamwua kwa kumupiga mawe. Ndivyo Waisraeli walivyofanya kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.

Currently Selected:

Walawi 24: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

Video for Walawi 24