Yoeli 4
4
Mungu atayahukumu mataifa
1Kwa wakati ule, na katika siku zile
nitakapowarudisha tena watu wa Yuda na Yerusalema
katika hali yao ya mbele,
2nitayakusanya mataifa yote,
niyapeleke katika bonde linaloitwa:
“Yawe anahukumu”.
Huko nitayahukumu mataifa hayo,
kwa mambo waliyowatendea watu wangu Waisraeli,
hao wanaokuwa mali yangu mimi mwenyewe.
Maana waliwatawanya kati ya mataifa,
waligawanya inchi yangu
3na kugawanya watu wangu kwa kupiga kura.
Waliuzisha vijana wanaume kwa kuhonga kahaba,
na wabinti kwa kupata divai.
4Munataka nini juu yangu enyi watu wa Tiro na Sidona na maeneo yote ya Filistia? Munataka kunilipiza kisasi? Kama munalipiza kisasi, mimi nitawalipiza mara moja! #Ang. Isa 14.29-31; 23.1-18; Yer 47.1-7; Eze 25.15–28.26; Amo 1.6-10; Zef 2.4-7; Zak 9.1-7; Mat 11.21-22; Lk 10.13-14 5Mumetwaa feza na zahabu yangu, na kuvibeba vitu vyangu vya bei kali mpaka kwenye mahekalu yenu. 6Mumewapeleka watu wa Yuda na Yerusalema mbali na inchi yao, mukawauzisha kwa Wagriki. 7Sasa, nitawarudisha watu wangu kutoka kule mulikowauzisha. Nitawalipiza kisasi kwa yote muliyowatendea. 8Nitawauzisha watoto wenu wanaume na wanawake kwa watu wa Yuda, nao Wayuda watawauzishia watu wa Seba, watu wa taifa la mbali kabisa.
–Ni Yawe anayesema hivyo.
9Muwatangazie watu wa mataifa jambo hili:
Mujitayarishe kwa vita,
muwaite mashujaa wenu;
waaskari wote wakusanyike,
waende mbele.
10Mufue majembe yenu kuwa mapanga,
visu vyenu vikubwa vikuwe mikuki.
Hata yule anayekuwa zaifu aseme:
“Mimi vilevile ni shujaa”. #Ang. Isa 2.4; Mika 4.3
11Mukuje upesi, enyi mataifa yote jirani,
mukusanyike kule katika bonde.
Ee Yawe!
Telemusha waaskari wako kuwashambulia!
12Mataifa haya yajiweke tayari;
yakuje kwenye bonde la Yawe Anahukumu.
Kule, mimi Yawe,
nitaikaa kwa kuyahukumu mataifa yote jirani.
13Mutwae kisu cha kuvuna,
maana sasa ni wakati wa mavuno.
Muingie! Muwapondeponde kama zabibu
ambazo zimejaza kikamulio.
Uovu wao umepita kipimo
kama mitungi inayofurika. #Ang. Ufu 14.14-16,19-20; 19.15
14Wanafika makundi kwa makundi
kwenye bonde la Hukumu,
maana siku ya Yawe imekaribia.
15Jua na mwezi vinatiwa giza,
na nyota zimeacha kuangaza.
Mungu atawabariki watu wake
16Yawe ananguruma kule Sayuni;
sauti yake inavuma kutoka Yerusalema;
mbingu na dunia vinatetemeka.
Lakini Yawe ni kimbilio la watu wake,
ni kikingio cha usalama kwa Waisraeli. #Ang. Amo 1.2
17Hapo, enyi Waisraeli,
mutajua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu,
ninakaa Sayuni, mulima wangu mutakatifu.
Muji Yerusalemu utakuwa muji mutakatifu;
na wageni hawatapita tena ndani yake.
18Wakati ule, divai mupya itatiririka juu ya milima,
na maziwa yatatiririka juu ya milima.
Vijito vyote vya Yuda vitajaa maji;
chemichemi itatokea ndani ya nyumba ya Yawe,
na kulinyweshea bonde la Sitimu.
19Misri itakuwa matongo,
Edomu itakuwa jangwa tupu,
kwa sababu waliwashambulia watu wa Yuda
wakawaua watu wasiokuwa na kosa.
20Lakini inchi ya Yuda itakaliwa na watu kwa milele,
na Yerusalema kwa kizazi hata kizazi.
21Nitawaazibu waliomwanga damu ya watu wa Yuda
wala sitawaachilia wenye makosa.
Yawe anakaa Sayuni.
Currently Selected:
Yoeli 4: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.