Amosi UTANGULIZI
UTANGULIZI
Amosi aliishi mbele ya manabii wengine wote ambao tumeachiwa vitabu vyao. Yeye alizaliwa katika ufalme wa kusini wa Yuda lakini akaitwa kutumika katika ufalme wa kaskazini katika mwaka 750 mbele ya Kristo.
Wakati huu ulikuwa wa fanaka na maendeleo ya uchumi na usalama. Lakini Amosi aliona kwamba hali hiyo ilipatikana kwa kutesa na kugandamiza wamasikini. Utimizaji wa mambo ya dini ulikuwa wa unafiki, na usalama wa kisiasa haukukuwa imara. Amosi alishitaki ukosefu wa haki katika taifa kwa uhodari wa pekee. Aliwaambia watu kwamba Mungu atawaazibu. Mwito wake kwa waongozi wapate kushika haki haukupokelewa vizuri. Alikatazwa kufanya kazi yake ya kinabii kule Beteli.
Currently Selected:
Amosi UTANGULIZI: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.