Yobu 25
25
1Kisha Bildadi wa inchi ya Suhi akajibu:
2Mungu ni mwenye uwezo mukubwa,
watu wote wamwogope.
Yeye anaweka amani mpaka juu kwake mbinguni.
3Nani anayeweza kuhesabu majeshi yake?
Ni nani asiyeangaziwa na mwangaza wake?
4Mutu anaweza basi namna gani kuwa mwenye haki mbele ya Mungu?
Mwanadamu tu anaweza namna gani kujidai kuwa safi?
5Kwake Mungu, hata mwezi hauangai vya kutosha,
nyota nazo si safi mbele yake;
6ni nini sasa mutu ambaye ni kidudu,
mwanadamu ambaye ni nondo tu!
Currently Selected:
Yobu 25: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.