Isaya 35
35
1Mbuga na inchi kavu vitachangamuka,
jangwa litafurahi na kuchanua maua.
2Litachanua maua kwa wingi kama waridi,
litashangilia na kuimba kwa furaha.
Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni,
uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni.
Watu watauona utukufu wa Yawe,
watauona ukubwa wa Mungu wetu.
3Muimarishe mikono zaifu,
mukaze magoti yanayoregea. #Ang. Ebr 12.12
4Muwaambie waliovunjika moyo:
Mujipe moyo, musiogope!
Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi,
atakuja kuwaazibu waadui zenu;
atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.
5Hapo vipofu wataona tena,
na viziwi watasikia tena. #Ang. Mat 11.5; Lk 7.22
6Viwete watarukaruka kama paa,
na bubu wataimba kwa furaha.
Maji yatabubujika katika jangwa
na vijito katika mbuga.
7Muchanga wa moto katika jangwa utakuwa ziwa la maji,
inchi kavu itabubujika vijito.
Makao ya imbwa wa pori yatajaa maji;
nyasi zitaota na kukomaa kama mianzi.
8Humo kutakuwa barabara kubwa,
nayo itaitwa Njia Takatifu.
Watu wachafu hawatapitia humo,
lakini wale watu wa Mungu tu;
wapumbafu hawatakanyaga ndani yake,
9humo hamutakuwa simba,
nyama yeyote mukali hatapitia humo,
hao hawatapatikana humo.
Lakini waliokombolewa ndio watakaopita humo.
10Waliokombolewa na Yawe watarudi,
watakuja Sayuni wakipiga vigelegele.
Watakuwa wenye furaha ya milele,
watajaliwa furaha na shangwe;
huzuni na kilio vitatoweka kabisa.
Currently Selected:
Isaya 35: SWC02
Highlight
Copy
Compare
Share
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.