Hosea 14
14
1Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao;
wamemwasi Mungu wao.
Watauawa kwa upanga,
watoto wao watapondwapondwa,
na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo.
Kumurudilia Mungu na hali mupya
2Enyi Waisraeli,
mumurudilie Yawe, Mungu wenu.
Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.
3Muombe huruma kwake,
mumurudilie na kumwambia:
Utusamehe uovu wote,
upokee zawadi zetu,
nasi tutakusifu kwa moyo.
4Inchi ya Asuria haitatuokoa,
hatutategemea tena farasi wa vita.
Hatutaziita tena Mungu wetu
hizo sanamu tulizochonga.
Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.
5Yawe anasema:
Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu;
nitawapenda tena kwa moyo wangu wote,
maana sitawakasirikia tena.
6Nitakuwa kama umande kwa Waisraeli
nao watachanua kama mayungiyungi,
watakuwa na mizizi kama muti wa mwerezi wa Lebanoni.
7Vichipukizi vyao vitazaa sana,
uzuri wao utakuwa kama mizeituni,
harufu yao nzuri kama maua ya Lebanoni.
8Watarudi na kuishi chini ya ulinzi wangu,
watastawi kama bustani nzuri.
Watachanua kama muzabibu,
harufu yao nzuri kama ya divai ya Lebanoni.
9Enyi watu wa Efuraimu,
muko na maneno gani tena na sanamu?
Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu,
mimi ndiye ninayewatunza.
Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi;
kutoka kwangu mutapata matunda yenu.
10Yeyote anayekuwa na hekima aelewe mambo haya,
mutu anayekuwa na akili ayatambue.
Maana njia za Yawe ni zenye kunyooka;
watu wa haki wanazifuata,
lakini wenye zambi wanaanguka katika njia hizo.
Currently Selected:
Hosea 14: SWC02
Highlight
Share
Compare
Copy
Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.