Kutoka 1
1
Waisraeli wanateswa katika inchi ya Misri
1Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli#1.1 Israeli: jina jingine la Yakobo (ang Mwa 32.29) jina ambalo nyuma lilikuwa jina la wazao wa Yakobo: Waisraeli. ambao walikwenda Misri, kila mumoja na jamaa yake: 2Rubeni, Simeoni, Lawi, Yuda, 3Isakari, Zebuluni, Benjamina, 4Dani, Nafutali, Gadi, na Aseri. 5Wazao wote wa Yakobo walikuwa watu makumi saba.#1.5 makumi saba: tafsiri ya Kigriki: makumi saba na watano; vilevile na maandiko mamoja ya Kiebrania yaliyopatikana kule Kumurani. Hesabu hiyo vilevile inatajwa katika Mdo 7.14 (ang vilevile Mwa 46.27). Wakati ule Yosefu alikuwa amekwisha kutangulia kukaa kule Misri.
6Kisha, Yosefu akakufa, vilevile na wandugu zake na kizazi kile chote. 7Lakini wazao wa Israeli wakaongezeka sana, wakakuwa wengi na wenye nguvu sana, wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri. #Ang. Mdo 7.17
8Basi, kukatokea mufalme mwingine#1.8 mufalme mwingine: labda yule alikuwa mufalme wa Misri Ramesesi II (1304-1238 mbele ya Kristo). kule Misri ambaye hakumujua Yosefu. 9Naye akawaambia watu wake: “Muangalie jinsi Waisraeli wanavyokuwa wengi na wenye nguvu kuliko sisi. 10Ni lazima tutafute werevu wa kuwapunguza na kuzuia wasiongezeke; kama sivyo, vita ikitokea watajiunga na waadui zetu na kutoroka#1.10 kutoroka: au: kutawala. inchi.”
11Basi, Wamisri wakachagua wakubwa wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumujengea mufalme wa Misri miji ya kuwekea akiba, Pitomu na Ramesesi. 12Lakini kadiri walivyoteswa ndivyo Waisraeli walivyozidi kuongezeka na kuenea katika inchi. Hivyo Wamisri wakawaogopa sana watu wa Israeli. 13Basi, Wamisri wakawatumikisha Waisraeli kwa kinguvu. 14Wakayafanya maisha yao kuwa magumu kwa kazi ngumu ya kutengeneza chokaa na kufyatua matofali, na kazi zote za shamba. Katika kazi zile zote, Waisraeli walitumikishwa kwa kinguvu.
15Kisha, mufalme wa Misri akawaambia wazalishaji wa Misri, Sifra na Puha, ambao waliwazalisha wanawake Waebrania: 16“Munapofanya kazi ya kuzalisha wanawake Waebrania, ikiwa mutoto anayezaliwa ni mwanaume, mumwue. Ikiwa ni mwanamuke, mumwache aishi.” 17Lakini kwa sababu wazalishaji wale walimwogopa Mungu, hawakufanya kama vile walivyoamuriwa na mufalme, lakini waliwaacha watoto wanaume wa Waisraeli waishi. 18Basi, mufalme akawaita wazalishaji wale, akawauliza: “Kwa nini mumefanya hivyo? Mbona mumewaacha watoto wanaume waishi?”
19Wao wakamujibu mufalme wa Misri: “Wanawake wa Waebrania si sawa na wanawake Wamisri. Wao ni hodari; mbele muzalishaji hajafika, wao wanakuwa wamekwisha kuzaa.”
20Basi, Mungu akawajalia mema wazalishaji wale, nao Waisraeli wakazidi kuongezeka na kuwa na nguvu sana. 21Na kwa sababu wazalishaji wale walimwogopa Mungu, Mungu akawajalia kupata jamaa zao wenyewe.
22Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.” #Ang. Mdo 7.19
Currently Selected:
Kutoka 1: SWC02
Highlight
Share
Copy

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in
Bible in Swahili Congo © Bible Society of the Democratic Republic of Congo (DRC), 2002.