YouVersion Logo
Search Icon

Kumbukumbu la Sheria UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu hiki kinaitwa Kumbukumbu la Sheria (Kumbukumbu la Torati katika tafsiri nyingine) kwa sababu kinarudilia tena sheria na maagizo Waisraeli waliyopewa kule kwenye mulima Sinai. Kitabu chenyewe kina masimulizi matatu ambayo Musa aliwaambia Waisraeli (1.1–4.43; 4.44–28.68 na 28.69–30.20). Musa anayataja mambo Mungu aliyoyafanya kwa ajili ya watu hao kutokana na upendo wake mukubwa: alifanya agano nao, aliwaongoza muda wote katika jangwa, aliwalinda na kuwakinga na waadui zao, akawapa amri na maagizo yake pamoja na ahadi zake. Musa anawasihi watu wakuwe waaminifu kwa Mungu na kuchagua kuwa na uhushirika mwema naye. Maneno makubwa yanayoandikwa katika kitabu hiki na yanayorudiliwa katika Matayo 22.37 ni haya: “Basi musikilize, enyi Waisraeli, Yawe, Yawe tu ni Mungu wetu. Mumupende Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote, kwa roho yenu yote na kwa nguvu yenu yote.” (6.4-5).
Katika sura ine za mwisho, ni kusema 31-34, kuna maandiko mawili ya kishairi na masimulizi mawili: tunaambiwa juu ya mwongozo na mashauri mbalimbali ambayo Musa aliwapa watu mbele ya kufa kwake. Musa anamuchagua Yoshua ashike nafasi yake (sura 31), wimbo wa Musa (sura 32), Musa anayabariki makabila 12 ya Israeli (sura 33), na mwisho habari za kifo cha Musa (sura 34).

Highlight

Share

Compare

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in