YouVersion Logo
Search Icon

Zab 36

36
Uovu wa Watu na Wema wa Mungu
Kwa mwimbishaji. Ya Daudi, mtumishi wa Bwana
1 # Rum 3:18; Mwa 20:11; Mit 8:13; Mhu 12:3 Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake,
Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.
2Kwa maana hujipendekeza machoni pake
Kuwa upotovu wake hautaonekana na kuchukiwa.
3 # Yer 4:22 Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila,
Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.
4 # Mik 2:1; Isa 65:2 Huwaza maovu kitandani pake,
Hujiweka katika njia mbaya; ubaya hauchukii.
5 # Zab 57:10 Ee BWANA, fadhili zako zafika hata mbinguni,
Uaminifu wako hata mawinguni.
6 # Ayu 11:8; Rum 11:33; Ayu 7:20; Zab 145:9 Haki yako ni kama milima ya Mungu,
Hukumu zako ni vilindi vikuu,
Ee BWANA, unawaokoa wanadamu na wanyama.
7 # Rut 2:12 Ee Mungu, jinsi zilivyo na thamani fadhili zako!
Wanadamu huukimbilia uvuli wa mbawa zako.
8 # Ayu 20:17; Ufu 22:1 Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako,
Nawe utawanywesha mto wa furaha zako.
9 # Isa 12:3; Yer 2:13; Zek 13:1; Yn 4:10,14; Ufu 21:6; Mdo 26:18; Efe 5:8; Kol 1:13; 1 Pet 2:9 Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima,
Katika nuru yako tutaona nuru.
10 # Yer 22:16 Uwadumishie wakujuao fadhili zako,
Na wanyofu wa moyo uaminifu wako.
11Mguu wa kiburi usinikaribie,
Wala mkono wa wasio haki usinifukuze.
12Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu;
Wameangushwa chini wasiweze kusimama.

Currently Selected:

Zab 36: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy