YouVersion Logo
Search Icon

Kum 34

34
Kifo cha Musa na Kuzikwa kwake katika Moabu
1 # Yos 19:40-48; Amu 18:28 Musa akapanda kutoka uwanda wa Moabu mpaka mlima Nebo, hata kilele cha Pisga kukabili Yeriko. BWANA akamwonyesha nchi yote ya Gileadi hata Dani; 2#Kut 23:31; Hes 34:6; Kum 11:24; Yos 15:12na Naftali yote, na nchi ya Efraimu na Manase, na nchi yote ya Yuda, mpaka bahari ya magharibi; 3#Amu 1:16; 3:13; 2 Nya 28:15na Negebu, na uwanja wa bonde la Yeriko, mji wa mitende, hata mpaka Soari. 4#Mwa 12:7; 26:3; 28:13BWANA akamwambia, Hii ndiyo nchi niliyowaapia Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, nikisema, Nitawapa wazao wako. Basi nimekuonyesha kwa macho yako, lakini hutavuka huko. 5#Kum 32:50; Yos 1:1,2; Mal 4:4Basi Musa, mtumishi wa BWANA, akafa huko, katika nchi ya Moabu, kwa neno la BWANA. 6#Yud 1:9Akamzika bondeni, katika nchi ya Moabu, kukabili Beth-peori; lakini hapana mtu ajuaye kaburi lake hata leo. 7#Kum 31:2; Mwa 27:1; 48:10; Yos 14:10Musa alikuwa mtu wa miaka mia na ishirini alipokufa; jicho lake halikupofuka, wala nguvu za mwili wake hazikupunguka. 8#Mwa 50:3; Hes 20:29; 1 Sam 25:1; Isa 57:1; Mdo 8:2Wana wa Israeli wakamwombolezea Musa katika uwanda wa Moabu siku thelathini; basi siku za maombolezo ya matanga ya Musa zikaisha. 9#Kut 31:3; Hes 11:17; 1 Fal 9:12; Isa 11:2; Dan 6:3; Hes 27:18Na Yoshua, mwana wa Nuni, alikuwa amejaa roho ya hekima; maana Musa alikuwa amemwekea mikono yake juu yake; wana wa Israeli wakamsikiliza, wakafanya kama BWANA alivyomwamuru Musa. 10#Kut 33:11; Kum 18:15,18; Hes 12:6; Kum 5:4Wala hajainuka tena katika Israeli nabii kama Musa, ambaye BWANA alimjua uso kwa uso; 11katika ishara zote na maajabu yote, ambayo BWANA alimtuma kuyatenda katika nchi ya Misri, kwa Farao, na kwa watumishi wake wote, na kwa nchi yake yote; 12na katika ule mkono wa nguvu wote, tena katika ule utisho mkuu wote, alioutenda Musa machoni pa Israeli wote.

Currently Selected:

Kum 34: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy