1
Mezali 13:20
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.
Compare
Explore Mezali 13:20
2
Mezali 13:3
Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.
Explore Mezali 13:3
3
Mezali 13:24
Asiyemwazibu mutoto wake hamupendi; lakini anayemupenda mwana wake atamwazibu kwa wakati.
Explore Mezali 13:24
4
Mezali 13:12
Tumaini la kungojangoja linaumiza moyo, lakini tazamio linalotimia ni musingi wa uzima.
Explore Mezali 13:12
5
Mezali 13:6
Haki inalinda wenye mwenendo sawa, lakini zambi inaangusha waovu.
Explore Mezali 13:6
6
Mezali 13:11
Mali ya harakaharaka inatoweka, lakini anayekusanya kidogokidogo ataiongeza.
Explore Mezali 13:11
7
Mezali 13:10
Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.
Explore Mezali 13:10
8
Mezali 13:22
Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.
Explore Mezali 13:22
9
Mezali 13:1
Mutoto mwenye hekima anasikia maagizo ya baba yake, lakini mwenye kiburi hasikilizi maonyo.
Explore Mezali 13:1
10
Mezali 13:18
Umasikini na mazarau vinamupata yule asiyejali mafundisho, lakini mwenye kusikia maonyo anaheshimiwa.
Explore Mezali 13:18