1
Matayo 27:46
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Ilipokuwa karibu saa tisa, Yesu akalalamika akisema: “Eli, Eli, lama sabaktani,” maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
Compare
Explore Matayo 27:46
2
Matayo 27:51-52
Na saa ile ile pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Inchi ikatetemeka, mawe makubwa yakapasuka, makaburi yakafunguka, na watakatifu wengi waliokufa zamani wakafufuliwa.
Explore Matayo 27:51-52
3
Matayo 27:50
Lakini Yesu, akalalamika tena kwa sauti kubwa na kukata roho.
Explore Matayo 27:50
4
Matayo 27:54
Mukubwa wa waaskari na wale waliokuwa pamoja naye wakimuchunga Yesu walipoona tetemeko la inchi na mambo yote yaliyofanyika, wakaogopa sana, na kusema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.”
Explore Matayo 27:54
5
Matayo 27:45
Tangia saa sita ya muchana, giza lilikuwa katika inchi yote mpaka saa tisa.
Explore Matayo 27:45
6
Matayo 27:22-23
Pilato akawauliza tena: “Basi munataka nifanye nini na huyu Yesu anayeitwa Kristo?” Nao wote wakajibu: “Atundikwe juu ya musalaba!” Pilato akawauliza tena: “Yeye alifanya ubaya gani?” Lakini wakazidi kupiga kelele wakisema: “Atundikwe juu ya musalaba!”
Explore Matayo 27:22-23
Home
Bible
Plans
Videos