1
Yeremia 8:22
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Hakuna dawa ya kupakaa kule Gileadi? Hakuna muganga kule? Mbona basi watu wangu hawajaponyeshwa?
Compare
Explore Yeremia 8:22
2
Yeremia 8:4
Wewe Yeremia utawaambia kwamba: Yawe anasema hivi: Mutu akianguka, hasimami tena? Mutu akipotea, harudii tena katika njia yake?
Explore Yeremia 8:4
3
Yeremia 8:7
Hata korongo anajua wakati wa kuhama; njiwa, mbaruwayi na koikoi, wanajua nyakati zao za kurudi. Lakini hawa watu wangu hawajui maagizo ya Yawe.
Explore Yeremia 8:7
4
Yeremia 8:6
Mimi nilisikiliza kwa uangalifu, lakini wao hawakusema ukweli wowote. Hakuna mutu anayetubu uovu wake, wala kujiuliza hivi: Nimefanya nini? Kila mumoja wao anashika njia yake, kama farasi anavyokimbia haraka kwa vita.
Explore Yeremia 8:6
5
Yeremia 8:9
Wenye hekima kati yenu wanafezeheka, watahangaishwa na kunaswa. Wamelikataa neno la Yawe. Basi ni hekima gani wanayokuwa nayo?
Explore Yeremia 8:9