Yawe anasema hivi:
Alaaniwe mutu anayemutegemea mwanadamu,
mutu ambaye anategemea nguvu za mwanadamu,
mutu ambaye moyo wake umegeuka mbali nami Yawe.
Huyo ni kama kichaka katika jangwa,
hataona mazuri yoyote.
Ataishi pahali penye kukauka katika jangwa,
kwenye udongo ulioharibiwa na chumvi,
na usiokaliwa na watu.