1
Yeremia 18:6
BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
SWC02
Enyi Waisraeli! Mimi siwezi kuwafanya ninyi kama mufinyanzi huyu anavyofanya? –Ni ujumbe wa Yawe.– Mujue kwamba kama vile udongo unavyokuwa katika mikono ya mufinyanzi, ndivyo ninyi munavyokuwa katika mikono yangu.
Compare
Explore Yeremia 18:6
2
Yeremia 18:7-8
Wakati wowote ninaweza kukusudia juu ya taifa au ufalme kwamba nitaliongoa, kulipindua na kuliangamiza. Lakini taifa hilo likigeuka na kuacha uovu wake, basi, mimi nitaacha kulitendea mambo yale niliyokusudia.
Explore Yeremia 18:7-8
3
Yeremia 18:9-10
Vilevile inaweza kunifikia kukusudia wakati wowote juu ya taifa au ufalme fulani kwamba nitalijenga na kulistawisha. Lakini taifa hilo likifanya uovu mbele yangu na kukataa kunitii, basi, mimi nitaacha kulitendea mema hayo niliyokusudia.
Explore Yeremia 18:9-10