Wageni watakaoshikamana nami Yawe,
kwa kunitumikia na kwa kupenda jina langu,
na kuwa watumishi wangu,
wote watakaoshika siku ya Sabato bila kuichafua,
watu watakaofuata agano langu,
hao nitawaleta katika mulima wangu mutakatifu,
na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya maombi;
sadaka zao na sadaka za kuteketezwa zitakubaliwa kwenye mazabahu yangu.
Maana nyumba yangu itaitwa:
Nyumba ya maombi kwa ajili ya watu wote.